Uchimbaji visima: Moïse Katumbi anahusika
Kujazwa zaidi kwa kuchimba visima ni mada ya mjadala kwenye mitandao ya kijamii. Ju ya Moïse Katumbi katika mawasiliano kupitia X (Twitter), kutolewa kwa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu na Waziri wa Fedha, Nicolas Kazadi, kulifanyika kinyume na masharti ya sheria ya ununuzi wa umma.
Kulingana na uzoefu wake, mpinzani na mfanyabiashara anaripoti kwamba bei ya wastani ya kutekeleza mradi wa kuchimba visima ni dola elfu makumi mbili (20) ya Amerika.
"Nimekamilisha zaidi ya visima miya tano (500) katika taaluma yangu, gharama ya kawaida kwa moja ni chini ya $20,000. Pesa zinakwenda wapi? ", aliuliza.
Katika mchakato , rais wa Ensemble pour la République anashangaa namna ulegevu wa mfumo wa sheria wa Kongo katika kuchunguza ufujaji wa fedha hizi, ambao mara zote umekuwa mwepesi wa kuwaweka wapinzani gerezani.
“cheria ya Kongo, ambayo ni ya haraka sana kuwashughulikia wapinzani, inakaa kimya. Ufisadi na ubadhirifu wa fedha za umma unazua maswali motomoto. Wahusika ni wani? Wakongo wanadai majibu na vikwazo vikali ju ya wale waliopanga ulaghai huu. Ni wakati wa uwazi kamili," aliongeza.
Waziri wa Fedha, Nicolas Kazadi, alitoa dola milioni makumi saba n'a moja(71 )kwa ajili ya ujenzi wa visima 1,000 katika maeneo ya vijijini. Kulingana na takwimu hizi, kisima kimoja cha kuchimba visima kiligharimu dola za Kimarekani 297,000