DRC: Augustin Kabuya anajiondoa kwenye kinyang'anyiro cha makamu wa rais wa Bunge la Kitaifa
Augustin Kabuya hatakuwa tena mgombea wa makamu wa rais wa Bunge la Kitaifa. Alitangaza uamuzi wake Siku ya pili hii, Aprili taré kenda katika makao makuu ya chama chake cha kisiasa.
Alisema alichukua uamuzi zaidi ju ya "kutekeleza vyema jukumu lake kama mlinzi wa serikali na kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kuhifadhi mamlaka ya UDPS."
Kulingana na vyanzo vilivyo karibu na chama cha urais, UDPS kitasimamisha mgombea mwingine kwa fasi hii.
Naibu wa kitaifa Augustin Kabuya alitangaza ugombeya fasi ya makamu wa kwanza wa rais wa Bunge la Kitaifa wakati wa asubuhi ya kisiasa iliyofanyika Machi taré kumi katika makao makuu ya chama.