Vita Mashariki: Paul Kagame anasema ndiyo kwa kupambana uso kwa uso na Félix Tshisekedi
Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Paul Kagame, alikaribishwa na mwenzake wa Angola na mwezeshaji wa mgogoro wa usalama mashariki mwa DRC, João Lourenço, Jumatatu mwezi wa tatu taré kumi na moja huko Luanda, mji mkuu wa Angola.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Angola, Munyerwanda Paul Kagame alikubali kukutana na Félix Tshisekedi kwa ajili ya mazungumzo kuhusu hali ya usalama mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mvutano kati ya Kinshasa na Kigali.
Mahali na tarehe ya mkutano kati ya Tshisekedi na Kagame itabidi iamuliwe na mkuu wa nchi wa Angola.
Muda mrefu kabla ya hapo, Rais João Lourenço alikuwa ametoa hadhira kwa mwenzake wa Kongo huko Luanda ju ya iyo uyo sababu . Félix Tshisekedi alihitika ndiyo ju ya mkutano na adui yake, Paul Kagame.