Haut-Katanga 1: Kuzinduliwa kwa michezo ya fani mbalimbali kati ya ma shule mbalimbali iliyotangazwa Jumamosi ijayo, Novemba taré ine
Mashindano ya fani mbalimbali baina ya shule ilianza rasmi Jumamosi hii, Novemba taré ine 2023, katika jimbo la elimu la Haut-Katanga 1.
Mashindano hayo yalizinduliwa na mshauri wa waziri wa elimu wa mkoa, Alain Kami katika uwanja wa michezo wa Kiwele.
Mkurugenzi wa elimu wa jimbo la Haut-Katanga 1 Joseph Mwinkeu Tshiend katika hotuba yake aliwaalika wanafunzi watakaoshiriki changamoto hii kutumia vyema kipindi chote cha michezo hiyo ili wakue na kushamiri kwenye mpango wa michezo. .
Katika siku hii ya kwanza, mechi ya kwanza kabisa ilizikutanisha timu ya wanawake kutoka shule ya Malaika katika tarafa ya Lubumbashi 4 dhidi ya ile ya shule ya Njanja katika tarafa ya tatu ya Lubumbashi. Matokeo yalimalizika kwa sefuru upande wote.