Kinshasa: Zaidi ya wa Kuluna elfu moja (1000) waliwasilishwa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani
Jumla ya majambazi 1,237 wa mijini wanaoitwa "Kuluna", waliwasilishwa kwa Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Ndani, Jumanne kwenye uwanja wa Mashahidi na kamishna wa kitengo cha jiji la Polisi la Kitaifa ya Kinshasa.
Peter Kazadi amewaahidi majambazi hawa kuwa hatakuwa na maelewano juu ya uhalifu waliofanya dhidi ya raia wenye amani, kabla ya kutangaza kuwa watafikishwa mahakamani Jumatano hii kujibu kwa matendo yao.
“Unachofanya Kuluna ni kutojiamini. Unaua, unabaka, unaiba... Sitakuwa na huruma hata na mtu anayeua, anayebaka. Kuanzia kesho, utawasilishwa mbele ya waamuzi wako wa asili kuhukumiwa na kujibu kwa matendo yako. Nyie ni raia nje ya jamii, hamuipendi congo na wala hamuwapendi Wacongomani. Ni lazima
tuwachukulie hivyo,” alisemeya Wakuluna.
Miongoni mwa kuluna hawa, pia kuna wahusika wa polisi ambao walikuwa na tabia mbaya.
“Binafsi nitakuchunga baada ya kukutwa na hatia. Utapelekwa gerezani, Angenga, Buluwo, sio Kinshasa. Kwa wa jambazi wengine, tunasema kwamba hatutawahi kuwaacha Wakuluna n'a Amani , kwa sababu habatshezake serikali, "aliendelea.
Apa Kinshasa, hakuna siku inayopita bila kitendo cha uharibifu unaosababishwa na vikundi vya vijana wajambazi.