DRC: Mpinzani Jean-Marc Kabund anahukumiwa kifungo cha miaka saba(7 ) ya jela
Hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi imeshuka. Naibu wa kitaifa Jean-Marc Kabund amehukumiwa kifungo cha miaka saba gerezani Jumatano hii, Septemba kumi na tatu, 2023.
Mpinzani huyo alipatikana na hatia ya mashtaka kadhaa yaliyoletwa ju yake. Uamuzi wa Mahakama ni mkali maradufu kuliko hati ya mashtaka ya Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Umma ambayo, wakati wa kusikilizwa kwa Agosti kumi n'a iné, iliomba miaka tatu ya utumwa wa adhabu ju ya Jean-Marc Kabund.
Jumla ya malalamiko kumi n'a mbili yamemkabili aliyekuwa makamu wa kwanza wa rais wa Bunge. Jean-Marc Kabund anashutumiwa hasa kwa kutoa "maneno ya matusi" dhidi ya mtu wa Félix Tshisekedi, mpenzi wake wa zamani.
Mahakama ya Cassation ilichanganya hukumu za makosa yote dhidi ya aliyekuwa makamu wa kwanza wa rais wa Bunge.
"Kwa kumkosea Mkuu wa Nchi, miezi minne, kueneza uvumi wa uwongo, miezi kumi na sita. Kwa kila kosa, Mahakama ilihifadhi hukumu, ilifanya limbikizo,” alisema Maître Kadi Diko, wakili wa Kabund.
Aliendelea kuwa "hukumu ni kali, miezi makumi nane na ine(84) ni kali".