Mauaji ya Goma: “Waandamanaji waliandamana dhidi ya sheria; Ndio msingi wa kilichotokea”, Peter Kazadi
Majukumu yanagawanywa kati ya askari wa Jeshi la Jamhuri na waandamanaji, baada ya mauaji ya wanachama wa dhehebu la Wazalendo huko Goma. Hivi ndivyo Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Ndani, Usalama, Ugatuaji na Mambo ya Kimila anaamini.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa taré sita Septemba , VPM Kazadi Peter alikumbuka hali ya utawala wa kuzingirwa katika jimbo la Kivu Kaskazini ambayo inakataza maandamano ya kiwango hiki.
“Waandamanaji waliandamana kinyume na sheria. Ndio msingi wa kilichotokea, ulichokiita uchinjaji wa binadamu. Kwa hili, lazima pia wahukumiwe kama wanajeshi walioteleza,” alisema VPM Kazadi.
Serikali inaweka mbali uwezekano wowote wa amri ya kupigwa risasi kwa wanajeshi na uongozi, kama ambavyo vuguvugu kadhaa za raia zinaamini. Peter Kazadi anazungumza kuhusu "Kuteleza kunakotokea kila mahali, hata Marekani."
Peter Kazadi na Patrick Muyaya wakisubiri hitimisho la kesi ya wazi ya askari hao iliyoanza katika Mahakama ya Kijeshi ya Goma, matokeo ya uungwana wa ujumbe wa serikali katika eneo la mauaji.
Peter Kazadi pia alikataa moja kwa moja habari iliyoambatanishwa na picha zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, kuhusu uwezekano wa kushambuliwa kwa dhehebu hilo pa saa ine asubuhi na askari wa kitengo cha wasomi.
Watu makumi tano wali uwawa Agosti taré makumi tatu huko Goma wakati wa maandamano yaliyokandamizwa sana ya madhehebu ya Wazalendo ambayo yalilazimishwa kuondoka kwa MONUSCO na jeshi la kikanda la EAC.