DRC: Félix Tshisekedi alizindua huduma kwa bure ya uzazi na watoto wanaozaliwa
Ilikuwa katika hospitali ya kijeshi ya Camp Tshatshi katika jiji la Kinshasa ambapo Rais wa Jamhuri, Félix-Antoine Tshisekedi Tshilombo, alizindua huduma ya uzazi na watoto wachanga bila malipo Jumanne hii.Septemba tare tano.
Hatua hii iliyozinduliwa na raia wa kwanza wa congo inakuja kujibu Ku matatizo ya kifedha ambayo wanawake wengi wanakutanaka nayo wakati wa kujifungua. Lengo ni kupunguza kiwango cha vifo vya wanawake wakati wa uzazi.
"Wanawake wajawazito, wale ambao wamejifungua na watoto wachanga watapata huduma bora za afya bila malipo bila matatizo ya kifedha kuwa kikwazo, na hii kwa ufadhili wa serikali," alisema Rais wa Jamhuri.
Kama sehemu ya mpango wa kwanza wa huduma kwa ajili ya utekelezaji wa Huduma ya Afya kwa Wote nchini DRC, uzazi wa mtoto bila malipo na matunzo ya watoto wachanga yataenea katika mikoa mbalimbali ya nchi, ikiwa ni pamoja na Kwilu.
"Pia tunafanya kazi kuhakikisha huduma hii bora ya afya inatolewa kwa majimbo ya Kwilu, Kasaï, Kasaï ya Kati, Kivu Kusini na mikoa mingine nane ifikapo mwisho wa mwaka. Mnamo 2024, utekelezaji wa kitaifa utakamilika, "alimhakikishia Rais Tshisekedi.
Ilikuwa ni mbele ya mamlaka kadhaa akiwemo Waziri wa Afya ya Jamii, Dk Roger Kamba, sherehe hii ilifanyika katika hali ya utulivu.
Kulingana na chanzo, likizo ya bure ya uzazi inaweza kuendelea hadi mwezi wa kwanza baada ya kuzaliwa kwa mtoto mchanga.