Kinshasa: Fally Ipupa atatoa tamasha kubwa mnamo taré sita mwezi Wa nane kando ya kufungwa kwa michezo ya Francophonie.
Ni msanii wa muziki Fally Ipupa ambaye amechaguliwa ju kucheza wakati wa kufunga toleo la tisa la Michezo ya La Francophonie mnamo Agosti taré sita katika esplanade ya Palais du Peuple huko apa Kinshasa.
Bango la msanii huyo tayari linazunguka kwenye mitandao ya kijamii. Tamasha kubwa litaanza saa kumi na mbili jioni (saa za Kinshasa) kando ya usiku wa Francophonie".
Kamati ya Kitaifa ya Michezo ya Francophonie ilikuwa imeahidi kuwashirikisha wasanii wakubwa wa muziki katika mkutano huu mkuu wa utamaduni na michezo wa Nchi Wanachama wa Shirika la Kimataifa ya Francophonie.
Ni msanii gani atatumbuiza kwenye sherehe za ufunguzi wa Michezo hiyo kwenye uwanja wa Mashahidi? Kamati ya Kitaifa ya Michezo ya Francophonie ilikuwa imeahidi kufanya mshangao mzuri kwa umma.