DRC: Serikali inachukua hatua ya kuruhusu ndege za Kongo kuruka eneo la Schengen
Mashirika ya ndege ya Kongo yanaweza kuona ndege zao zikiruka juu ya baadhi ya anga za kimataifa ikiwemo Schengen. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Uchukuzi, Mawasiliano na Ufikiaji wakati wa mkutano wa Oktoba kumi na sita.
Ju ya Marc Ekila, Waziri wa Uchukuzi, hii ingeruhusu nchi kujiondoa kwenye orodha isiyoruhusiwa ya Umoja wa Ulaya.
"Mamlaka ya usafiri wa anga tayari iko kwenye mazungumzo na mashirika ya Ulaya, ambayo ni kusema tayari tunajaza fomu ili kuruhusu ndege za Kongo kuingia eneo la Schengen," alisema.
Pia alifahamisha kwa waandishi wa habari kwamba nchi imevuka wastani wa Afrika katika suala la viwango baada ya ukaguzi wa ICAO (Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga) kuwa 55.9.
"Leo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kufuatia ukaguzi wa ICAO ambao ulifanyika kutoka Februari tare moja hadi tare kumi mwaka huu, tumetoka na rating iliyothibitishwa na 64.56%", aliongeza.
Kuhusu kufilisika kwa shirika la ndege la Congo Airways, Marc Ekila alisema kuwa serikali inajitahidi kuwapatia wananchi wa Kongo ndege ili kuhakikisha wanasafiri, huku akitaja taratibu ndefu za upatikanaji wa ndege hizo.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inakabiliwa na ukosefu wa ndege kwa makampuni yake ya ndege. Ndege zote zinazomilikiwa na serikali hazina uwezo tena wa kuruka.