DRC: Mradi wa miaka mitano ya Moise Katumbi uligharimu dola bilioni miya makumi ine na moja
Mara baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri mnamo Desemba tare makumi mbili, Moïse Katumbi anaahidi budget inayokadiriwa kuwa dola bilioni miya makumi ine na moja kwa miaka yake mitano katika ofisi kuu.
Mradi wa utawala wa chama cha siasa cha Ensemble pour la République 2024-2028 uliwasilishwa kwa vyombo vya habari Jumatatu hii, Novemba kumi na tatu , 2023 na mmoja wa wana mawasiliano, Christian Mwando, aliyekuwa Waziri wa Mipango.
Mpango wa utawala wa mgombea wa upinzani Moïse Katumbi unajumuisha malengo kumi na moja, ikiwa ni pamoja na kuboresha hali ya maisha ya watu, afya, usalama, diplomasia na kilimo.
Mara tu atakapoingia madarakani, anaona budget ya dola za Marekani bilioni 1.4 ili kuongeza malipo ya mahakimu, gharama za uendeshaji wa mahakama na ujenzi wa mahakama.
Gavana wa zamani wa jimbo la zamani la Katanga pia anapanga kuunda kanda za kilimo, ukarabati wa barabara za kilimo, msaada kwa wanawake wa kilimo na maendeleo ya kilimo cha mkataba. bilioni 7.1 za budget zitatengwa kwa ajili ya sekta ya kilimo.
Mpango huu wa 2024-2028 wa Moïse Katumbi unaitwa « Mbadala wa 2024 kwa Kongo iliyoungana, ya kidemokrasia, yenye mafanikio, yenye haki na iliyoungana ».