Uvamizi wa nguvu na tshama ya maendeleo ya UDPS kwa Kabila: « waliwatuma waje kuniondoa kimwili », Olive Lembe.
Mbele ya waandishi wa habari, mke wa rais wa heshima, Olive Lembe Kabila alieleza kukerwa kwake na uvamizi usio na mafanikio wa kikosi cha UDPS kwenye moja ya manyumba yake huko Gombe.
Olive Lembe anaona nyuma ya kitendo hiki nia ya makusudi « ya wanamgambo wa UDPS kumuondoa kimwili.»
« Nitatoa wito kwa mamlaka kuhusu hatari inayowakilishwa na wanamgambo hawa wa UDPS wanaodumishwa kwa bahati mbaya. Inaonekana ni huduma sambamba ambayo inafanya kazi badala ya Serikali. Haiheshimu Jamhuri,» alisema.
Zaidi ya mia moja wanatshama kutoka UDPS Force du Progres walivamia mbele ya makazi ya Rais wa zamani Joseph Kabila. Milio ya risasi iliripotiwa wakati wa makabiliano haya na walinzi wa Joseph Kabila. Mkewe Olive Lembe alikuwepo wakati wa tukio. Polisi wanasema wamewakamata takriban wanachama kumi wa Force du Progres.
