Uchokozi wa Rwanda: « Mkuu wa Nchi aliajiri wanaume na kuwapa vifaa vya kukabiliana na vita hiyi », Vital Kamerhe

Rais wa Jamhuri, Félix-Antoine Tshisekedi Tshilombo, alitoa hotuba kwa Rais wa Bunge la Kitaifa, Vital Kamerhe, Jumatano Agosti taré Saba jioni katika jiji la OAU apa Kinshasa. 

Redaction

8 mwezi ya nane 2024 - 15:02
8 mwezi ya nane 2024 - 15:03
 1
Uchokozi wa Rwanda: « Mkuu wa Nchi aliajiri wanaume na kuwapa vifaa vya kukabiliana na vita hiyi », Vital Kamerhe

Mazungumzo kati ya watu hawa wawili yalihusu masuala ya siku hizo, ikiwa ni pamoja na vita ya uvamizi ya Rwanda katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. 

"Mkuu wa Nchi hakupuuza njia. Aliajiri wanaume, akawafunza na kuwapa vifaa vya kukabiliana na vita hiyi,” Vital Kamerhe alisema.

Rais wa Jamhuri na mwenyeji wake pia walijadili masuala ya kiuchumi ya nchi, hasa kushuka kwa thamani ya faranga ya Kongo dhidi ya sarafu ya Marekani, dola. 

“Rais wa Jamhuri anaonya wauzaji wa jumla wote wanaotoza bei za kudhalilisha. Udhibiti katika sekta hii utakuwa wa kawaida na wa kina (…) Ni wakati wa mpango wa mabadiliko na mseto wa uchumi wa taifa letu kutekelezwa na kuwepo na ufuatiliaji wa kudumu,” aliongeza. 

Kwa mujibu wa vyombo vya habari ya rais, mkutano kati ya Rais wa Jamhuri, Rais wa Bunge na mkuu wa serikali umepangwa hivi karibuni kuchunguza masuala ya nchi .

Redaction UNE.CD est un média en ligne basé à Kinshasa, capitale de la République Démocratique du Congo, qui collecte, traite et diffuse des informations générales de la RDC, l'Afrique et le Monde. Grâce à nous, l'actualité vous suit partout en temps réel sur votre téléphone, tablette et ordinateur en un seul clic.