Urais: Mahakama ya kikatiba yathibitisha kuchaguliwa tena kwa Félix Antoine Tshisekedi
Katika hali isiyo ya kushangaza, Mahakama ya Kikatiba ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imemthibitisha hivi punde Félix Antoine Tshisekedi kama rais aliyechaguliwa tena kwa asilimia 73.47 ya kura.
Alikuwa Rais wa Mahakama ya Kikatiba, Dieudonné Kamuleta, ambaye alitangaza moja kwa moja kwenye televisheni ya taifa jioni ya Jumanne, Januari taré kenda.
Baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa na CENI, ni zamu ya mahakama ya kikatiba kutoa uamuzi ili kukamilisha mchakato huu wa uchaguzi Desemba 2023.
Mahakama pia itatoa uamuzi kuhusu kesi za ukiukwaji wa sheria zilizobainishwa na kukashifiwa na upinzani na viongozi fulani wa maoni.