Uchaguzi wa ubunge wa kitaifa na majimbo: wagombea makumi nane na mbili (82) wamebatilishwa kwa udanganyifu akiwemo Ngobila, Tshomba, Pululu na Bakonga
Jumla ya wagombea makumi nane na mbili ( 82 ) katika uchaguzi wa wabunge wa kitaifa, mkoa na manispaa walibatilishwa na tume huru ya taifa ya uchaguzi (CENI) kwa udanganyifu, uharibifu, uchochezi wa vurugu na kuwekwa kizuizini kinyume cha sheria kwa DEV (Kifaa cha Kupigia Kura) akiwemo Gentiny Ngobila, Colette Tshomba , Nsingi Pululu na Willy Bakonga.
Haya yalitangazwa na kituo cha uchaguzi katika matangazo ya moja kwa moja ya televisheni ya taifa ya DRC, jioni ya Ijumaa Januari taré tano,2024.
Wagombea awa waliobatilishwa wanashutumiwa, pamoja na mambo mengine, kwa udanganyifu, rushwa, ujazo wa kura, kumiliki vifaa vya kupigia kura kinyume cha sheria (DEV) na vitisho kwa mawakala wa CENI.
Miongoni mwa wanaume na wanawake hao waliobatilishwa na ushawishi mkubwa wa kisiasa, kuna hasa wanachama wa Umoja wa Kitaifa (Jukwaa la kisiasa la Rais wa Jamhuri), UDPS, familia ya kisiasa ya rais na wengine wengi walio karibu na mamlaka.
Haya hapa ni majina ya baadhi ya wagombea hawa makumi nane na mbili waliobatilishwa: