Jean-Luc Melenchon kwa Tshisekedi: « Nasubiri tu hukumu ya Ufaransa kuleta ju ya Rwanda »
Mpinzani wa Ufaransa Jean-Luc Melenchon alipokelewa na Rais wa Jamhuri, Félix-Antoine Tshisekedi Tshilombo, Alhamisi hii, Oktoba makumi mbili na sita 2023. Majadiliano kati ya Mkuu wa Nchi na kiongozi wa « France insoumise » yalibadilisha kuhusu uchaguzi ujao na uvamizi wa Rwanda nchini DRC.
Kwa vyombo vya habari, mwanasiasa huyo wa Ufaransa alifahamisha kwamba anasubiri kukomeshwa kwa huosama wa Rwanda katika ardhi ya Kongo, akitumai kwamba kulaaniwa kwa Ufaransa kuta gusa zamiri ya nchi ya Paul Kagame .
« Nasubiri kulaaniwa kwa Ufaransa, kupitia azimio lililowasilishwa na wenzangu, ili kuirejesha Rwanda pamoja. DRC inatamani amani na kuandaa uchaguzi wake inavyoona inafaa. Tunataka Rwanda iacha malengo yake ya kujitanua,» alisema.
Akisindikizwa na manaibu wachache kutoka kwa familia yake ya kisiasa, Jean-Luc Melenchon hakuficha kutoridhishwa kwake na uvamizi wa Wanyarwanda katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wakiandaa uchaguzi.
« Wanaibu hawa wametia saini pendekezo mbele ya bunge la Ufaransa ambalo linalaani uvamizi na unyanyasaji unaofanywa na Rwanda nchini DRC,» aliongeza.
Mwanasiasa wa Ufaransa Jean-Luc Melenchon amekuwa akiishi Kinshasa tangu Jumanne iliyopita, Oktoba makumi mbili na tatu. Atashiriki katika mkutano katika UNIKIN (Chuo Kikuu cha Kinshasa) katika siku za usoni.