Kinshasa: Katumbi, Fayulu, Matata na Sesanga waahirisha maandamano yao Ku taré makumi mbili mwezi wa Tano
Viongozi wa upinzani Moïse Katumbi, Martin Fayulu, Augustin Matata Ponyo na Delly Sesanga wameamua kuahirisha maandamano yao ya amani hadi Ku taré makumi mbili mwezi wa tano, 2023 apa Kinshasa, mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya congo.
Tangazo hilo lilitolewa na viongozi Awa wanne wa upinzani mbele ya waandishi wa habari walipokuwa wameamua kuendeleza maandamano yao Ku taré kumi n'a tatu , hivyo kupinga uamuzi wa Gentiny Ngobila.
Maandamano haya yaliahirishwa kwa mara ya kwanza hadi Ku taré kumi n'a nane kwa idadi ya jiji la Kinshasa, kabla ya kudumishwa kwa taré kumi n'a tatu na upinzani wenyewe, ambao hatimaye uliamua kuahirisha hadi mwezi wa Tano taré makumi mbili.
Moïse Katumbi, Martin Fayulu, Augustin Matata Ponyo na Delly Sesanga wataandamana dhidi ya gharama ya juu ya maisha, mchakato wa uchaguzi wenye machafuko na usawazishaji.