DRC: Sama Lukonde alimtangazia Kalehe ju ya kuwahurumia wahanga
Ujumbe wa serikali unaoongozwa na Waziri Mkuu, Jean-Michel Sama Lukonde Kyenge, unatarajiwa katika siku chache katika eneo la Kalehe, katika jimbo la Kivu Kusini. Hii, ili kuwahurumia waathiriwa na familia zilizoachwa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha Alhamisi, taré iné, mwezi wa Tano na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali na kupoteza maisha ya watu.
Kwa mujibu wa Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Usalama, Ugatuzi na Mambo ya Kimila aliyetangaza kwa waandishi wa habari baada ya kikao kilichoongozwa na Sama Lukonde, serikali ya Jamhuri inafuatilia kwa karibu magumu yoote ya Kalehe.
“Mkuu wa Serikali alisisitiza kinachoendelea Kalehe. Unajua, tulikumbana na janga la kibinadamu kutokana na mvua kubwa iliyosababisha uharibifu wa mfumo wa ikolojia na vifo vya zaidi ya watu miya ine. Hatua zitatangazwa hivi karibuni kwenye mstari wa kufuata kuhusiana na hali hii. Lakini tayari, uju