DRC: barua mpya ya waendesha gari itapatikana mwishoni mwa 2024 [Jean-Pierre Bemba]
Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Jean-Pierre Bemba alikuwa na kikao cha kazi na Bob Amiso, Waziri wa Uchukuzi wa Mkoa wa Kinshasa, Agosti makumi mbili na nane katika mji mkuu wa Kongo.
Kwa mujibu wa taarifa tulizonazo, Jean-Pierre Bemba alimtangazia mwenyeji wake kuwa serikali kuu inaweka juhudi yote katika kuwapatia wananchi barua mpya ya udereva.
Kwa upande wake, Waziri wa jimbo Bob Amiso alimweleza VPM Jean-Pierre Bemba azma yake ya kuweka huduma ya usafiri ya jiji ya Kinshasa kwenye kidijitali, ili kuhakikisha usalama barabarani na kutatua matatizo kadhaa katika sekta hii.
Ukarabati wa reli
Msongamano kubwa ambayo imeikumba Kinshasa hivi majuzi haijawatoroka mawaziri hao wawili. Jean-Pierre Bemba na Bob Amiso walikubali kukarabati reli hiyo iliyoko Avenue belgika
Ju ya kufanya hivyo, Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Uchukuzi na Waziri wa Uchukuzi wa Mkoa waliamua kufanya kazi kwa pamoja ju kufanikisha mradi huu ambao unalenga kuunganisha katikati ya jiji na magharibi mwa Kinshasa.
Mradi huu unafuata nyayo za Kin Metro, mradi ambao pia unalenga kuboresha trafiki katika jiji ili kuepuka msongamano wa magari katika mji mkuu.
