Christophe Lutundula Kuusu Wazalendo: "hatuwezi kumlaumu Mkongomani anayechukua silaha ju ya kutetea nchi yake"
Akikubiliana na waandishi wa habari Jumatatu Oktoba makumi mbili na ine wakati wa taarifa hiyo, Naibu Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Nje alikaribisha mashambulizi ya vijana wazalendo wanaokabiliana na magaidi wa M23.
Christophe Lutundula anaamini kwamba "hatuwezi kumlaumu Mkongomani ambaye anachukua silaha ju ya kutetea nchi yake" katika uso wa tishio la uadilifu wa eneo kama lile lililofanywa na jeshi la Rwanda chini ya ulinzi wa M23.
Waziri wa Mawasiliano na Vyombo vya Habari, katika utangulizi wake, alionyesha picha za vyombo vya habari zilizochukuliwa na ndege zisizo na rubani za MONUSCO zikiwaonyesha wanajeshi wa Rwanda katika mji la Tongo huko Kivu Kaskazini ili kuwaongezea nguvu magaidi wa M23 wanaoteseka kutokana na mashambulizi ya vijana.wazalendo.
Kinshasa inashikilia msimamo wake kuhusu kuheshimu usitishaji mapigano kama ilivyokubaliwa katika ramani ya barabara ya Nairobi na majadiliano ya Luanda. Serikali ya Kongo inalaumu, zaidi ya yote, jirani yake Rwanda, ambayo inaendelea kuwaua raia mashariki mwa DRC.