Urais 2023: Moïse Katumbi ashughulikia "ma ahadi ambazo hazijatekelezwa" za Tshisekedi pale Moanda
Jumanne, Septemba makumi mbili na sita, rais wa Ensemble pour la République, Moïse Katumbi, alitembelea mkoa wa Kongo- ya kati, magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Ziara ya mgombea urais wa Jamhuri ilianza katika mji wa Moanda. Mwenyekiti huyo alipokelewa na bahari ya watu waliohamia uwanja wa ndege wa jiji hilo. Katika hotuba yake, Moïse Katumbi aliashiria ahadi ambazo hazijatekelezwa na Rais Tshisekedi katika upande uyu wa nchi.
"Muanda lazima afanane sawa Monaco. Faranga ya Kongo inashuka huku mishahara haifuati. Lazima tuwe na bateaux za uvuvi hapa. Mafuta ni hapa, lakini mrahaba haufuati. Kongo-Kati ni mji mkuu wa sasa. Pia imebarikiwa na mafuta. Mkoa hauwezi kuwa maskini. Itaisha baada ya miezi miwili,” alisema.
Gavana wa zamani wa jimbo la zamani la Katanga pia alielezea nia ya kuandaa CAN (Kombe la Mataifa ya Afrika) na CHAN (Mashindano ya Mataifa ya Afrika) katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, mara tu atakapochaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri.
Baada ya Moanda, Moïse Katumbi alikwenda katika mji jirani wa Boma. Umati mkubwa pia uliitikia kwa wingi wito wa chama cha Ensemble pour la République.
Katika Kongo-katikati, kama katika majimbo mengine aliyopita, Moïse Katumbi alihubiri kufufuliwa kwa chama chake cha kisiasa na maono yake ya Kongo, ikiwa atachaguliwa kuwa Rais.