Uchaguzi wa 2023: Noël Tshiani anashambulia ugombea wa Moïse Katumbi katika Mahakama ya Kikatiba ju ya kukosa utaifa.
Vyanzo kadhaa vya habari vinatangaza ombi la Noël Tshiani kwa Mahakama ya Kikatiba la kubatilisha ugombea wa Moïse Katumbi, hasa kwa kukosa uraia asili wa Kongo.
Kulingana na wataalamu fulani wa vyombo vya habari, mgombea urais alitoa ushahidi mahakamani kama vile makala kutoka vyombo vya habari vya Ufaransa JeuneAfrique iliyochapishwa mwezi Wa tatu 2018 ili kupata ubatilishaji wa kesi ya mpinzani Moïse Katumbi.
Katika kambi ya Moïse Katumbi, majibu kutoka kwa jiji la SAN VITO DEI NORMANI kukana kusajiliwa kwa Moïse Katumbi katika rejista ya raia wa Italia, yanazunguka kwenye mitandao ya kijamii, kwa kujibu Noël Tshiani.
Mjadala kuhusu asili na utaifa wa Moïse Katumbi unapamba moto kwenye mitandao ya kijamii. Huku wakisubiri ugombea wake uitikwe au uidhinishwe na mahakama, watu wake wanasema wako tayari kuingia mitaani endapo ugombea wake utabatilishwa.