Mkutano wa makumi ine n'a tatu wa SADC: Felix Tshisekedi anaomba kuandaliwa kwa "Michezo ya SADC" na "Miss SADC"
Mjini Luanda Alhamisi hii, Agosti taré kumi na Saba 2023 katika mkutano wa makumi ine na tatu ya Wakuu wa Nchi na Serikali ya SADC, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya congo aliomba kuandaliwa kwa mashindano ya shirika la kikanda la vijana.
Mkuu wa Nchi ya congo alipendekeza kuandaliwa kwa michezo ya SADC na mashindano ya Miss SADC ambalo, kulingana na yeye, litaongeza kasi ya udugu kati ya vijana wa nchi tofauti wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika.
"Furaha ya kizazi chetu hakika itakuwa kubwa zaidi siku ambayo shughuli za kitamaduni jumuishi, kama "Miss SADC", "Michezo ya SADC" itaharakisha udugu kati ya watoto wetu na wajukuu zetu katika mipaka yetu, katika eneo lenye amani na ustawi kabisa. " alisema.
Félix Tshisekedi Tshilombo ambaye aliwaalika washiriki kujiunga na wazo lake, alisema anatumai "kwamba watoto wanaweza kuishi katika Mkoa bora zaidi kuliko ule tuliorithi kutoka kwa Waanzilishi wetu".
Angola ni mwenyeji wa Mkutano wa 43 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC ambao umeanza Alhamisi hii chini ya kaulimbiu "Binadamu na Fedha: Vichochezi muhimu vya Uendelezaji wa Viwanda Endelevu katika Kanda ya SADC".