DRC: Serikali inakusudia dola bilioni 13 katika mapato mnamo 2026
Serikali ya Kongo inakusudia kupandisha mapato ya umma kwa dola bilioni 13 mnamo 2026, ju ya bilioni 9,9 ilizotolewa tayarishwa katika sheria ya fedha ya 2025.
Uamuzi huu ulifanywa, Jumanne, Agosti 19, baada ya mkutano wa kufanya kazi kati ya Naibu Waziri Mkuu anayesimamia budget, Adolphe Muzito; Waziri wa Fedha, Doudou Fwamba na Makamu wa Waziri wa budget Elysée Bokumwana.
Ju ya kufikia kwenye lengo hili ililoonekana kuwa la kutamani, mashirika ya kifedha yanaitwa kuongeza juhudi zao.
Mikutano ya budget ya Julai-Agosti ilikuwa imetoa makadirio ya dola bilioni 11 tu, chini ya mfumo wa budget wa kati uliosimamishwa kwa bilioni 11.7.
Kwa kuzingatia , Adolphe Muzito aliomba wa tawala kuvuka kizingiti hiki na kuchunguza hatua ya kuzidi bilioni 12.
Mkakati huyu ni sehemu ya hamu ya serikali ya kuongeza rasilimali ya ndani na kupunguza garama ya maisha. Mwaka jana, amri ilikuwa tayari imepunguza TVA kwenye bidhaa fulani muhimu.
Rolly Lengo, mkurugenzi wa DGPPB, alikumbuza ya kwamba uraia wa ushuru unabaki kuamua. Kwa yeye, walipa kodi wanapolipa ushuru na ushuru, serikali ina njia ya kufadhili shule, hospitali, barabara, mshahara na uendeshaji wa huduma ya umma.
